Friday, January 06, 2006

Jokes

Dealing with criminals

A local policeman had just finished his shift one cold November evening and was at home with his wife. "You just won't believe what happened this evening , in all my years on the force I've never seen anything like it." "Oh yes dear, what happened ?" "I came across two guys down by the canal, one of them was drinking battery acid and the other was eating fireworks." "Drinking battery acid and eating fireworks!! What did you do with them ?" "Oh that was easy, I charged one and let the other off."
Mabaharia watatu kortini kwa kuwatosa Watanzania baharini 2006-01-07 09:04:26 Na Johannesburg, Afrika Kusini
Mabaharia watatu wa Ukraine wamefikishwa mahakamani nchini Afrika Kusini kujibu mashtaka ya kuwatumbukiza baharini Watanzania waliokuwa wamezamia ndani ya meli yao. Watanzania wawili walikufa maji katika tukio hilo lililokea Jumatano iliyopita karibu na bandari ya Durban. Msemaji wa polisi mjini Durban Bi. Ugu Sabela alisema mabaharia hao na nahodha wa meli hiyo walifikishwa mahakamani jana. Alisema hata hivyo wameachiwa kwa dhamana ya dola 3,200 za Kimarekani. Bi. Sabela alisema kutoswa kwa Watanzania hao baharini kulikuja baada ya meli hiyo kuwasili mjini hapa ikitokea Mombasa nchini Kenya. Sheria za Afrika Kusini zinawataka wenye meli zilizowabeba wazamiaji kulipa gharama za kuwarejesha nchini mwao. Wazamiaji watano miongoni mwa saba waliweza kuogelea lakini wengine wawili walishinda na hatimaye kufa maji. Msemaji wa polisi alisema mabahari hao kila mmoja anashtakiwa kwa makosa mawili ya kuua na matano ya kujaribu kuua. Kwa upande wake nahodha anakabiliwa na mashtaka ya kusaidia kuwasafirisha wahamiaji haramu na kwamba kuna uwezekano pia wa kukabiliwa na mashtaka kuua na kujaribu kuuwa. Habari zilisema waokoaji bado hawajafanikiwa kuzipata maiti za Watanzania wawili walitoswa baharini. Polisi nchini Afrika Kusini, imesema tatizo la vijana kuzamia linazidi kuwa kubwa.

Silvery

Karibuni wote, ili tuweze kuelimishana juu ya mambo ya dunia hii.

Silvery